Lori latumbukia mtoni wakati madereva wakifukuza wezi

 Baadhi ya wananchi wakilishuhudi Lori hilo likiinuliwa kutoka kwenye mtaro
 Hatari wakati zoezi la kuliinua lori hilo likiendelea watoto hao walinaswa na kamera za Mtandao huu waliingi kwenye mtaro  wakisaka mafuta ya Petroli yaliomwagika kutoka kwenye lori hilo
 Vibaka hao walitumia ngazi hizi kupanda juu ya Lori hili na kushusha mizigo iliyokuwa juu ya Tenk
                                     Lori hilo baada ya kuinuliwa


Vijana hao wakitimu mbio baada ya kuona kamera za Mtandao huu zikiwamulika wakati wakizoa mafuta hayo.

NA DUSTAN SHEKIDELE,MOROGORO.
KATIKA hali ya kushangaza Lori la mafuta aina ya Scania lenye namba za usajiri T772 BAZ limetumbukia lenye bila dereva kwenye mtaro uliopo eneo la Kihonda barabara kuu ya Morogoro Dodoma baada ya dereva wa Lori hilo kushuka na kuliacha gari hilo bila kulizima na kuwafukuza wezi waliokuwa juu ya tenk la gari hilo wakishusha mizigo.

Shuhuda wa tukio hilo Bw Joseph Furahisha alipohojiwa na mtandao huub alisema

" Dereva wa Lori hili alipofika pele kwenye tuta alishuhudia pikipiki ikiwasha taa na kuzima  aliamua kuongeza umakini na kubani kwamba mmoja wa abiri aliyekuwa kwenye pikipiki hiyo alipanda juu ya Tenk na kushusha maboksi ya Oil ndipo dereva huyo aliposhuka fasta akajisahau kuvuta 'endbrack'hivyo wakati akiwafukuza wezi hao huku Lori hilo lililokuwa kwenye mtelemko lilitembea bila dereva na kuingia kwenye mtaro huu"alisema shuhuda huyo.

Dereva wa Lori hilo Bw ldd Hoza alipohojiwa na mwandishi wa habari hizi alisema  alikuwa akisafirisha mafuta ya petroli kutoka Dar es salaama kueleka Dodoma na kwamba alipofika kwenye daraja la Kihonda alipunguza mwendo kwa lengo la kulipanda tuta lililokuwa eneo hilo la daraja.

" Kwa kawadi dereva unapopunguza mwendo ni lazima uangalie kwenye kioo nyuma yako kuna nini hivyo nilipoangalia niliona dereva wa pikipiki akiwasha taa na kuzima nilipochunguza zaidi nikaona mtu yuko juu ya Tenk akishusha maboksi ya Oil nikashuka na kumfukuza kwakuwa eneo hili ni la mtelemko gari hili ilitembea yenye na kuingia kwenye mtaro na wezi hao walifanikiwa kuondoka na boksi moja la oil kwa kutumia pikipiki yao"alisema Dereva huyo ambaye mpaka muda huu huyo hapo eneo la Tukio
Chanzo: Shekidele

Author

Written by DK

Napenda kusafiri, hasa kutembelea kila mkoa katika nchi yangu nzuri Tanzania, nafanya hivyo maana hiyo ndio njia niliyochukua katika kutumikia taaluma yangu ya habari na mawasiliano ya umma

0 comments: