
Hali hiyo ilitokana na ratiba ya treni kutofuatwa na kusababisha
abiria waliozoea usafiri huo kurundikana huku kukiwa na sintofahamu juu
ya hatima yao.
Wakizungumza na Tanzania Daima, baadhi ya abiria wa treni hiyo
waliushutumu uongozi wa TRL na kudai kuwa wanamhujumu Waziri wa
Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe kwa kufanya mambo ya makusudi na
kumtaka waziri huyo kulitupia macho suala hilo.
“Hizi ni hujuma, watu wanajua treni halifanyi kazi toka saa tano
kwanini wasirekebishe na hata kuunga vichwa mapema ili watu wakija saa
10 jioni waondoke? Lakini wao wakifika muda huo sababu kibao,” alisema
mmoja wa abiria hao.
Kwamba wafanyakazi wa TRL waliendelea kukata tiketi kwa abiria licha
ya kufahamu kuwa treni haiondoki kwa wakati na tangazo la kuhairisha
safari ya treni hiyo iliyokuwa iondoke saa 10 jioni lilitolewa saa
10:15.
Hivi karibuni, Ofisa Habari wa TRL, Midladjy Maez, alikaririwa
akisema mabadiliko ya safari za treni jijini yametokana na ubovu wa
vichwa vya treni hiyo.
“Hii ni dharura na si kweli kama kuna mabadiliko ya ratiba… hakuna
hujuma zozote, changamoto yetu ni hitilafu katika vichwa hivyo,”
alisema Maez.
Chanzo: Tanzania Daima
0 comments: