Abiria watakiwa kukata tikeki mapema

BARAZA la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra CCC) limewataka abiria wanaosafiri katika msimu wa mapumziko ya Desemba kuhakikisha wanapata tiketi mapema ili kuepuka usumbufu.
Mkurugenzi wa Sumatra CCC, Oscar Kikoyo, alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana na kusema kuwa kutokana na wingi wa abiria kuna baadhi ya watoa huduma wasio waaminifu hupandisha nauli  bila kufuata kanuni.
Kikoyo alisema ni vema abiria kuwa na tabia ya kushirikiana na mamlaka zilizopewa jukumu kuhakikisha wanasafiri kwa usalama ili kukomesha vitendo vinavyohatarisha usalama na maisha yao.
Alisema usalama wa abiria ni muhimu kuliko safari yenyewe, hivyo ni wajibu wao kutoa taarifa bila woga wala kuhofia, ili kuepukana na vitendo vya ulaghai, kuuziwa tiketi za safari kwa bei juu, kupandishwa kwenye basi bovu na kubadilishiwa basi alilopangiwa kusafiri nalo.
Baraza hilo pia limewataka abiria wanaotumia usafiri wa treni inayotoa huduma kati ya Stesheni na Ubungo Maziwa na lile la Tazara–Mwakanga kuacha tabia ya kudandia pindi treni linapoanza safari.

Author

Written by DK

Napenda kusafiri, hasa kutembelea kila mkoa katika nchi yangu nzuri Tanzania, nafanya hivyo maana hiyo ndio njia niliyochukua katika kutumikia taaluma yangu ya habari na mawasiliano ya umma

0 comments: