Daladala Kimbiji zatakiwa kutoza 750/-


MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), imewataka madereva na makondakta kuwatoza abiria wanaosafiri kati ya Kigamboni hadi Kimbiji sh 750 badala ya sh 1,300.

Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya madereva na makondakta kupambana na abiria waliokuwa wakipinga nauli ya sh 1,300.
Akizungumza na wananchi pamoja na madereva jijini Dar es Salaam juzi, Ofisa Mfawidhi Kanda ya Mashariki, Conrad Shio, alisema hakuna haja kwa madereva hao kuzua mgogoro wakati kila kitu kiko wazi.
Alisema Sumatra imeamua abiria watozwe nauli ya sh 750 baada ya kubaini umbali wanaosafiri hauzidi kilomita  25.5.
“Kama kuna dereva na kondakta asiyetaka kuwatoza abiria hao ni vema akaondoa gari lake katika barabara hiyo,” aliema Shio.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kimbiji, Ubaya Abdallah, alisema madereva hao awali kabla kijiji hicho hakijaingizwa kwenye ramani ya Sumatra walikuwa wakitoza nauli sh 1,300.
Chanzo: Tanzania Daima

Author

Written by DK

Napenda kusafiri, hasa kutembelea kila mkoa katika nchi yangu nzuri Tanzania, nafanya hivyo maana hiyo ndio njia niliyochukua katika kutumikia taaluma yangu ya habari na mawasiliano ya umma

0 comments: