SUMATRA yakunjua makucha

Mamlaka ya Udhibiti, Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), imesitisha leseni za usafirishaji kwa mabasi yanayomilikiwa na Kampuni ya Osaka Royal Class, Polepole Classic na Burhan Bus Service.

Uamuzi huo umetokana na mabasi ya kampuni hizo, kuhusika kwenye ajali zilizotokea katika maeneo, siku tofauti ambapo watu walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa.
Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Meneja Mawasiliano wa SUMATRA, Bw. David Mziray, alisema Desemba 10 mwaka huu, basi la Osaka Royal Class lenye namba T819 BYL, lilipata ajali na kuua watatu na majeruhi 33.
Basi hilo lilikuwa likitoka Arusha kwenda Dar es Salaam na ajali hiyo ilitokea kwenye eneo la Kirinjiko, Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, ambapo chanzo cha ajali ni dereva wake kushindwa kulimudu na mwendo kasi.
“Kwa kuzingatia Kifungu namba 15 cha Sheria ya SUMATRA na pia Kanuni namba 22 ya Kanuni za Ufundi, Usalama na Ubora wa Huduma za mwaka 2008, Mamlaka imeamua kusitisha leseni za usafirishaji kwa mabasi yanayomilikiwa na kampuni hii.
“Mabasi hayo ni yenye namba T819BYL, T417 AAG, T852 AUL, T206 CJZ, T201 CJZ, T437 BJK na T852 AUL, yatapewa leseni za usafirishaji baada ya kutekeleza maagizo.
Maagizo hayo ni kuhakikisha mabasi ya kampuni hiyo ambayo namba zake zimetajwa, yakaguliwe na Mkaguzi kutoka Jeshi la Polisi na kuthibitisha kama yanakidhi viwango vya ufundi na usalama.
Madereva wa mabasi yaliyotajwa wajaribiwe na Jeshi la Polisi ili kujiridhisha kama wana sifa za kuendesha mabasi, kuwasilisha kwa maandishi mpango utakaotumiwa na kampuni kudhibiti ajali za barabarani zinazosababishwa na madereva wake.
Alisema Kampuni ya Polepole Classic, Desemba 8 mwaka huu, basi lenye namba T 898 BKN, lilipata ajali Kijiji cha Machangarawe, Wilaya ya Babati mkoani Manyara.
Ajali hiyo ilisababisha vifo vya watu watano na majeruhi 32 ambapo taarifa za Jeshi la Polisi zilisema chanzo cha ajali ni dereva kushindwa kuchukua tahadhari wakati akiendesha usiku na kuligonga trekta lililoegeshwa barabarani.
Aliongeza kuwa, SUMATRA ime amu a k u s i t i s h a l e s e n i za usafirishaji kwa mabasi yanayomilikiwa na kampuni hiyo katika njia ya Moshi-Babati yenye namba za usajili T898 BKN, T267AZL na T212BLZ.
Leseni za usafirishaji kwa magari hayo zitatolewa baada ya kukamilisha maagizo kama yaliyotolewa kwenye kampuni ya Osaka Rolay Class.
Bw. Mziray alisema Desemba 12 mwaka huu, basi la Kampuni ya Burdani Bus Service, lenye namba T610 ATR likitokea Korogwe kwenda Dar es Salaam, lilipata ajali Kijiji cha Taula, Wilaya ya Handeni na kusababisha vifo vya watu 12, majeruhi 93.
Basi hilo lilikuwa likiendeshwa na Bw. Ruta Kwadahel ambapo taarifa za jeshi zilisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi, uzembe wa dereva na kujaza abiria kupita kiasi.
SUMATRA imechukua hatua ya kusitisha leseni za usafirishaji kwa mabasi yanayomilikiwa na kampuni hiyo yenye namba T158BXG, T610ATR, T572BXJ, T994AGD na T607ATR.
Leseni za usafirishaji kwa magari hayo zitatolewa baada ya kampuni hiyo kukamilisha maagizo waliyopewa wenzao

Chanzo;Majira

Author

Written by DK

Napenda kusafiri, hasa kutembelea kila mkoa katika nchi yangu nzuri Tanzania, nafanya hivyo maana hiyo ndio njia niliyochukua katika kutumikia taaluma yangu ya habari na mawasiliano ya umma

0 comments: