Zaidi ya abiria 5,000 magari 100 yakwama eneo la Wami

ABIRIA zaidi ya 5,000 na magari madogo na makubwa 100 waliyokuwa wakisafiri kwenda mikoa ya kaskazin na waliokuwa wakija jijini Dar esalaama na Morogoro wamekwama kwa zaidi ya saa tatu leo Desemba mbili katika barabara kuu ya Chalinze Segera eneo la mto Wami wilayani Bagamoyo mkoani Pwani baada ya njia kufunga.

Tukio hilo limetokea majira ya saa tatu asubuhi desemba mbili baada ya magari mawili KAV 429/ ZA 5047 aina ya Benz na KBR 224 / ZB 1109 Benzi yaliyokuwa yaikitokea Kenya kwenda Burundi kushindwa kupandisha mlima na hivyo kurudi nyuma na kupinduka.

Katika tukio hilo moja kontena moja na Benzi liliangukia barabarani na hivyo kusababisha magari mengine yanayotumia njia hiyo kushindwa kupita kuendelea na safari hatua ambayo ilileta adha kubwa kwa abiria hasa wa mabasi waliokuwa wakienda mikoa ya Tangam Kilimanjaro,Arusha na Kenya , Daresalaam, Chalinze na Morogoro.

Diwani wa kata ya Mbwewe Madaraka Mbonde amedhibitisha kutokea adha hiyo ambapo amesema alifika eneo la tukio na kukuta maloro hayo yameanguka na hivyo kwa kushirikiana na askari polisi walibuni njia mbadala ya kuyawezesha magari mengine kupita na hivyo kulazimika kutengeneza njia ya vumbi pembezoni (daiveshen) mwa barabara kuu eneo la tukio ili kuyawezesha magari madogo na mabasi kuendelea na safari.

Amesema ubunifu huo uliwezesha zoezi la msururu wa magari kupita japo kwa tabu huku lori lililoanguka likisubir krein kuja kulinyanyua.

Mkuu wa usalama barabarani mkoani Pwani Nassor Sisiwaya amethibitsiha tukio hilo huku akitaja majeruhi wa ajali hiyo ni Mohamed Rashid (35) mkazi wa Tanga na kwamba  hali yake inaendelea vema.


Amesema Chanzo cha tukio hilo ni magari hayo mawili kufeli breki kisha kuanza kurudi nyuma na kuanguka na kuziba barabara eneo hilo la Wami.

Author

Written by DK

Napenda kusafiri, hasa kutembelea kila mkoa katika nchi yangu nzuri Tanzania, nafanya hivyo maana hiyo ndio njia niliyochukua katika kutumikia taaluma yangu ya habari na mawasiliano ya umma

0 comments: