Barabara za Johannesburg kufungwa kupisha shooting ya filamu ya The Avengers

Chanzo: Bongo5
Barabara kadhaa za katikati ya jiji la Johannesburg kuanzia leo Jumanne zitafungwa kupisha shooting ya filamu ya The Avengers.
the-avengers-1235-wallmages
Uchukuaji wa filamu hiyo utaanza saa 12 jioni hadi Jumatano asubuhi.

Mitaa mingine itafungwa kuanzia February 14 hadi 23. Mitaa itakayoathirika ni President Street kwenda Rissik na Eloff streets na Joubert Street kwenda Harrison na Rissik streets. Polisi wamesema sehemu za mitaa ya Commissioner, Sauer na Albetina Sisulu nayo itafungwa.
image  loading
Muendelezo wa filamu hiyo ya Hollywood, iliyopewa jina ‘Avengers: Age of Ultron’ utahusisha waigizaji maarufu wakiwemo Robert Downey Jr, Scarlett Johansson, Chris Evans na Chris Hemsworth.

Author

Written by DK

Napenda kusafiri, hasa kutembelea kila mkoa katika nchi yangu nzuri Tanzania, nafanya hivyo maana hiyo ndio njia niliyochukua katika kutumikia taaluma yangu ya habari na mawasiliano ya umma

0 comments: