Facts: Facebook imebadilisha utamaduni wetu wa kufanya safari



Mwezi huu Facebook imetimiza miaka kumi tangu kuanzishwa kwake na naweza kudhubutu kusema kuwa mtandao huu umekuwa ni miongoni mwa mitandao mikubwa na yenye mafanikio duniani

Mtandao huu umefanikiwa kubadilisha kwa kiasi kikubwa utamaduni wetu wa kupanga safari na kutembela maeneo mbalimbali, kwa ujumla naweza kusema kumekuwa na mafanikio na madhara ambayo yameletwa kama mabadiliko katika sekta ya usafiri nchini na dunia kote.

Mabadiliko yafuatayo yanaweza kueleza vizuri mchango wa facebook kwenye ulimwengu wa sasa wa usafiri.

Ndoto za kusafiri zinaweza kutimia: Ukiingia tu kwenye facebook na kukutana na picha za marafiki zako wakiwa wamepanda ndege (plane), farasi au basi au hata bodaboda, au wakionyesha wako katika hifadhi za taifa ni rahisi mno kwako wewe kuipata picha na kujiona tayari umeshafika eneo hilo, wakati mwingine waweza hata kuona wivu kwanini haujafika eneo hilo au kwanini mpenzi/mzazi/rafiki yako hajakupeleka huko.

Tunapata taarifa nyingi: Kupitia makundi na kurasa za marafiki na jamaa, ukiweka maswali yako yakiuliza ni wapi panafaa kutembelea au wapi unafikiria kutembelea wakati wa mapumziko au sikukuu basi marafiki watachangia mawazo na kukupa maelezo mengi tu, jambo linalokufanya usiku na mchana uendelee kuota ndoto za mahala hapo. wataaalmu wanasema kuwa kadri unavyokuwa na mawazo chanya juu ya kitu unachokipanga, furaha huongezeka na kukifanya kitu hicho kutoakea kweli.

Ushauri kutoka kwa marafiki zetu: Unapoweka nia yako ya kutaka kusafiri kwenda mahala na kutaka kupata maoni ya rafiki zako, kwa mfano "hoteli gani ni nzuri kwa familia mkoani Morogoro" hapa kila mtu atachangia kulingana na uzoefu wake na weledi na mwisho wa siku utapata ushauri utakaokusaidia katika safari yako.

Ukweli kwa haraka: Zamani ilikuwa ngumu kidogo ililazimika siku, miezi na pengine miaka ndio uweze ku-share uzoefu wako katika safari au kuonyesha ndugu jamaa na marafiki picha zako ulizopiga ukiwa kwenye matembezi fulani, lakini sasa mtu yuko mbugani anaweza kupiga picha na kuiweka facebook na marafiki zake kujionea kinachoendelea.

Kujua ulipo: Huu unaweza kuwa ni uzuri lakini unaweza kuwa ubaya pia wa facebook, maana unaponesha uko eneo fulani wakati mwingine inaweza kufichua jambo ambalo hukutaka lijulikane, mfano mzuri umetoroka nyumbani na kwenda na marafiki zao pahala na mkapiga picha na wenzako kuweka kwenye facebook, kuna hatari ya wazazi au ndugu, walimu au walezi kuona picha hizo na baadae kukushikisha adabu

Huondoa upweke: Japokuwa kwa sasa facebook kama inapoteza umaarufu wake lakini imekuwa iki-play great role katika kuondoa msongo wa mawazo na upweke, jambo ambalo mtu anaweza kuwasiliana na watu wengine na kubadilishana mawazo hata kama yuko mbali na familia akiwa safarini.

Uporaji: Wakati mwingine tunapotoa taarifa kwamba tuko kwenye mapumziko mahala pengine, wezi na majambazi hutumia nafasi hii kubomoa na kuiba majumbani kwetu hasa kama watu wenyewe wanatufahamu fika na pengine ni marafiki zetu facebook, unajua si rahisi kujua kila tabia ya rafiki yako wa facebook. 
Safari moja, kwa pamoja

Author

Written by DK

Napenda kusafiri, hasa kutembelea kila mkoa katika nchi yangu nzuri Tanzania, nafanya hivyo maana hiyo ndio njia niliyochukua katika kutumikia taaluma yangu ya habari na mawasiliano ya umma

0 comments: